KITAIFA: Brazil yaisamehe Tanzania mabilioni ya fedha ya mwaka 1979. Kamanda Mambosasa amtaka polisi anayejiita Faru john. Mwenyekiti wa serikali ya mtaa akamatwa na polisi baada ya kumkaribisha mkuu wa mkoa kwenye kikao cha kijiji akiwa amelewa. Bunge lahitimishwa watanzania wakishuhudia kheri na vitimbwi. Kina Manji wasomewa mashtaka saba wakiwa muhimbili. Sakata la mimba shuleni latua kwa ma-DC. Majaliwa: Marufuku kusafirisha chakula nje ya nchi. Bakwata yalaani mauaji Kibiti. JPM kuzindua viwanda Pwani leo katika ziara ya siku 3 inayoanza mkoani humo. Kamusi Kuu ya kiswahili yapitishwa Bungeni. ********** KIGAMBONI: Hali ya hewa ni ya baridi kiasi na upepo, wananchi washauriwa kuwa makini na upepo, vumbi wakati wa mchana na baridi wakati wa usiku. **********KIMATAIFA: Boti yazama, 6 wafa, 20 wakimbizwa hospitali Colombia. **********BIASHARA: Sekta ya Benki yaanza kuona nuru mpya. Rangi itakuongezea au kukupunguzia wateja katika biashara yako. Mazingira ya biashara yaboreshwe kukuza uchumi, kuondoa umasikini. Shilingi 50 yaanza kupoteza bidhaa za kuendananazo baada ya wafanyabiashara wengi kutengeneza zaidi vitu vya shilingi 100. *********MICHEZO: *** UEFA: Timu za EPL zaanza vyema mzunguko wa kwanza. Diego Costa aachwa kwenye kikosi cha wachezaji 25 wa chelsea watakaoshiriki UEFA hatua ya makundi. Zlatan Ibrahimovic ajumuishwa kwenye kikosi cha wachezaji 25 wa Man United watakaoshiriki UEFA hatua ya makundi. Real Madrid bingwa. ENGLAND: Chelsea bingwa EPL, Conte achaguliwa kocha bora wa msimu. . ******** LA LIGA: Real Madrid bingwa la liga. ******* USAJILI: Lacazette kumfikirisha upya Sanchez juu ya kuihama Arsenal. Atletico yamtaka Diego Costa kutulia Chelsea hadi Januari.*********** AFRIKA: Ligi ya vilabu bingwa Afrika iko katika hatua ya makundi. AFCON 2017; Cameroon alitawazwa kuwa Bingwa baada ya kuifunga Misri goli 2-1 katika fainali na sasa inacheza kombe la mabara. ******** Pata habari hizi na nyinginezo nyingi kupitia habari zetu za michezo za kimataifa. ********. TANZANIA: *** Simba yazidi kufanya kweli. Msuva aipaisha TZ. TRA: Klabu za soka zilipe kodi. *** KIGAMBONI: Uhaba wa ligi ndani ya Wilaya ya Kigamboni umezorotesha uibuaji wa vipaji na kudumaza viwango vya wachezaji waliopo. Wadhamini waombwa kujitokeza kuanzisha ligi mbalimbali wilayani humo ili kuwaokoa vijana wengi na mambo mabaya. Katika uwanja wa Mnadani karibu na maeneo ya Tungi kwa kasilati ligi ambayo inakusanya wachezaji wengi kwa sasa imeisha kwa Mkunazini kuibuka bingwa katika fainali baada ya miaka mingi kupita. Ligi ya Eid El Fitr yaendelea katika hatua ya robo fainali leo 20/6/2017, katika uwanja wa machava.

Friday, November 4, 2016

TASWIRA YA MJI MPYA WA KIGAMBONI


image
image
image
image
image
image
image
image
image

Mambo yameiva kwa wakazi wa Kigamboni, hii ni sehemu ya majengo ya utakao kuwa mji mpya wa Kigamboni kwa mujibu wa Mtandao wa Wizara husika.
Eneo hili litahusu maeneo ya makazi yasasa ambayo yanakaliwa na watu. Kwa mujibu wa Tangazo la Serikali la Mwaka 2008 wakazi wa kata zipatazo tano watafidiwa kuhamishwa kupisha mradi huu.
Eneo litakalo chukuliwa ni la Kigamboni likichukua zaidi ya kata tano ambazo ni Kigamboni, Vijibweni, Somangila, Mji Mwema na Kibada. Eneo hili lina wakazi wapatao 82,808 ambao watafidiwa kulingana na sheria na taratibu zilizowekwa.
Mradi huu ukikamilika mwaka 2030 utakuwa ni mji wa kipekee si tu kwa Tanzania bali kwa Afrika pia.


Socializer Widget By Blogger Yard
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →

0 comments:

Post a Comment