KITAIFA: Brazil yaisamehe Tanzania mabilioni ya fedha ya mwaka 1979. Kamanda Mambosasa amtaka polisi anayejiita Faru john. Mwenyekiti wa serikali ya mtaa akamatwa na polisi baada ya kumkaribisha mkuu wa mkoa kwenye kikao cha kijiji akiwa amelewa. Bunge lahitimishwa watanzania wakishuhudia kheri na vitimbwi. Kina Manji wasomewa mashtaka saba wakiwa muhimbili. Sakata la mimba shuleni latua kwa ma-DC. Majaliwa: Marufuku kusafirisha chakula nje ya nchi. Bakwata yalaani mauaji Kibiti. JPM kuzindua viwanda Pwani leo katika ziara ya siku 3 inayoanza mkoani humo. Kamusi Kuu ya kiswahili yapitishwa Bungeni. ********** KIGAMBONI: Hali ya hewa ni ya baridi kiasi na upepo, wananchi washauriwa kuwa makini na upepo, vumbi wakati wa mchana na baridi wakati wa usiku. **********KIMATAIFA: Boti yazama, 6 wafa, 20 wakimbizwa hospitali Colombia. **********BIASHARA: Sekta ya Benki yaanza kuona nuru mpya. Rangi itakuongezea au kukupunguzia wateja katika biashara yako. Mazingira ya biashara yaboreshwe kukuza uchumi, kuondoa umasikini. Shilingi 50 yaanza kupoteza bidhaa za kuendananazo baada ya wafanyabiashara wengi kutengeneza zaidi vitu vya shilingi 100. *********MICHEZO: *** UEFA: Timu za EPL zaanza vyema mzunguko wa kwanza. Diego Costa aachwa kwenye kikosi cha wachezaji 25 wa chelsea watakaoshiriki UEFA hatua ya makundi. Zlatan Ibrahimovic ajumuishwa kwenye kikosi cha wachezaji 25 wa Man United watakaoshiriki UEFA hatua ya makundi. Real Madrid bingwa. ENGLAND: Chelsea bingwa EPL, Conte achaguliwa kocha bora wa msimu. . ******** LA LIGA: Real Madrid bingwa la liga. ******* USAJILI: Lacazette kumfikirisha upya Sanchez juu ya kuihama Arsenal. Atletico yamtaka Diego Costa kutulia Chelsea hadi Januari.*********** AFRIKA: Ligi ya vilabu bingwa Afrika iko katika hatua ya makundi. AFCON 2017; Cameroon alitawazwa kuwa Bingwa baada ya kuifunga Misri goli 2-1 katika fainali na sasa inacheza kombe la mabara. ******** Pata habari hizi na nyinginezo nyingi kupitia habari zetu za michezo za kimataifa. ********. TANZANIA: *** Simba yazidi kufanya kweli. Msuva aipaisha TZ. TRA: Klabu za soka zilipe kodi. *** KIGAMBONI: Uhaba wa ligi ndani ya Wilaya ya Kigamboni umezorotesha uibuaji wa vipaji na kudumaza viwango vya wachezaji waliopo. Wadhamini waombwa kujitokeza kuanzisha ligi mbalimbali wilayani humo ili kuwaokoa vijana wengi na mambo mabaya. Katika uwanja wa Mnadani karibu na maeneo ya Tungi kwa kasilati ligi ambayo inakusanya wachezaji wengi kwa sasa imeisha kwa Mkunazini kuibuka bingwa katika fainali baada ya miaka mingi kupita. Ligi ya Eid El Fitr yaendelea katika hatua ya robo fainali leo 20/6/2017, katika uwanja wa machava.

KARIBU UTUFAHAMU SISI NI AKINA NANI

Sisi ni kikundi cha vijana tunaoishi wilaya ya Kigamboni. Kwa muda mrefu tumekuwa na ndoto nyingi tofauti za maendeleo.
Tuliweza kukutana na kuwa na lengo moja, la kufanyia kazi ndoto zetu nzuri kwa kujitoa kikamilifu kwa hali na mali. Haikuwa kazi rahisi hata kidogo kuhakikisha tunakua pamoja.
Mnamo tarehe 1 mwezi wa 6 mwaka 2016 kikundi kilianza rasmi kikiwa na watu 8 kwa jina la Youth Unlimited Dream Exploration Group (YUDE).
Kikundi hiki kinashughulika na ndoto za vijana zinazolenga kuleta maendeleo katika jamii. Hivyo kwa pamoja YUDE ni kikundi cha vijana wanaothubutu kujishughulisha ama kutumia fursa zilizopo na kutengeneza nyingine kuleta maendeleo katika jamii kwa kutumia taaluma zao na vipawa vyao mbalimbali katika nyanja zote.

Malengo:
  • ·         Kuamsha vijana kutimiza ndoto zao kwa kujitoa kikamilifu.
  • ·         Kufanya miradi mbalimbali zaidi kwa kuhusisha teknolojia.
  • ·         Kuwa na mfumo mzuri wa taarifa kwa jamii.
  • ·         Kuleta mahusiano mazuri kati ya vijana na jamii.
  • ·         Kutumia fursa zilizopo katika jamii kuleta maendeleo.
Shughuli zetu:
  • ·         Kikundi.
Ø  Kutumia fursa za IT kama vile kutengeneza na kuiendesha mifumo mbalimbali (blog/ website, IT Systems), kufundisha na kushauri.
Ø  Kutumia fursa za ujasiliamali kufanya miradi mbalimbali na kuisadia jamii kupata elimu ya ujasiliamali.  
  • ·        Kijamii.
Tunajitoa kikamilifu kuisaidia jamii katika shughuli mbalimbali kama vile elimu, usafi na kutembelea wagonjwa ama wenye shida mbalimbali. Pia kutoa habari za matukio mbalimbali za ndani na nje ya jamii.

Miradi:
Ipo miradi ambayo inahitaji msaada wa hali na mali (Wasiliana nasi kwa maelezo zaidi).

Changamoto:
  • ·         Kutokua na mtaji wa kutosha.

Sehemu kubwa ya vijana hawana ajira, hivyo ni vigumu kutegemea kipato cha ndani pekee kutimiza malengo.
  • ·    Ugumu wa kuwapata vijana wote kwa wakati mmoja, kutokana na kazi zetu nyingi kuwa ni za kujitolea na zisizo na kipato cha kutosha.
  • ·         Mtazamo hasi wa wanajamii walio wengi juu ya vijana.
  • ·         Upungufu wa vitendea kazi hususani katika maswala ya Teknolojia (Kompyuta, kamera n.k)
  • ·         Ukosefu wa udhamini.
Maombi:
  • ·         Tunaomba misaada ya hali na mali katika fursa tunazozichukua.
  • ·         Tunapokea kazi za kibiashara kama vile ajira, fursa ya kuweka matangazo katika mitandao yetu n.k
  • ·         Tunakaribisha mawazo ama michango mbalimbali kutoka katika jamii.
Hitimisho:
Tunaomba ushirikiano zaidi kutoka kwa serikali, watu binafsi ama mtu yeyote mwenye mapenzi mema kiujumla.

0 comments:

Post a Comment